`

Home » » WANAFUNZI WAUNGANA NA WALIMU WAO KUANZISHA SHAMBA LA MFANO LA PAMBA

WANAFUNZI WAUNGANA NA WALIMU WAO KUANZISHA SHAMBA LA MFANO LA PAMBA


 
     wakulima katika shughuli zao za kilimo:                            
Wakulima wakiwa katika shughuli za kilimo cha pamba:


           Pamba iliyokomaa kabla ya kuvunwa:

          Pamba iliyovyunwa tayari kwa kupelekwa sokoni:
NA AHMAD NANDONDE RORYA.

Walimu pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Nyamasieki wilayani Rorya mkoani Mara wameanzisha shamba darasa la zao la Pamba kama sehemu ya kufanya majaribio ya kilimo cha zao hilo litakalokuwa likilimwa kwa njia ya kisasa na hivyo kuwasaidia wakulima wilayani humo kutafuta zao la biashara na hivyo kusaidia kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi kupitia zao hilo.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Nyamasieki Bw. PETER EXAVERY amesema baada kufanikiwa katika jaribio la kwanza la ulimaji wa zao hilo msimu uliopita uongozi na wanafunzi wa shule hiyo wameamua kuongeza hekari 21 ili kukiendeleza kilimo hicho.

Aidha ameongeza kuwa mapato yatokanayo na zao hilo yatasaidia kutatua mahitaji ya chakula kwa wanafunzi shuleni hapo.

Kufuatia ubunifu uliofanywa na viongozi na wanafunzi wa shule hiyo mwenyekiti wa umoja wa vijana CCM wilayani humo DAVID IRANGA amewaomba wananchi kuacha kulalamikia ugumu wa maisha na badala yake waige mfano ulioneshwa na shule hiyo ili kujikwamua kiuchumi.
Mwishoo...
 KILIMO NI AJIRA EWE MWANANCHI KIMBILIA FURSA HIII SASA:




0 comments:

Post a Comment

 
Designed By | Wishes co |
Copyright © 2014. Jicho La Mdadisi - All Rights Reserved
Template Modify by
Proudly powered by Wishes INK