`

Home » » CHAMA CHA MAPINDUZI CCM KATA YA KYENYARI WILAYANI BUTIAMA KUSOMESHWA BURE WATOTO ISHIRINI WALIOFAULU MTIHANI WA DARASA LA SABA.

CHAMA CHA MAPINDUZI CCM KATA YA KYENYARI WILAYANI BUTIAMA KUSOMESHWA BURE WATOTO ISHIRINI WALIOFAULU MTIHANI WA DARASA LA SABA.

Na Ahmad Nandonde,

Musoma.

JUMLA ya watoto wapatao ishirini waliofaulu mtihani wa darasa la saba na kushindwa kwenda shule kwa ukosefu wa ada katika kata ya kyenyari wilayani butiama wanataraji kusomeshwa bure katika elimu ya sekondari.

 Hayo yalisemwa jana na mjumbe wa mkutano mkuu kata ya kenyari ambaye pia ni mjumbe huyo wa halmashauri kuu ccm kwa upande wa vijana (uvccm) wilayani butiama bw. Mgingi Muhochi alipokuwa akiwahutubia wananchi wa kijiji cha mwibagi kata ya kyenyari wilayani butiama.

 Bw. Muhochi alisema ili kuendana na mpango wa serikali wa matokeo makubwa sasa (BRN) hivyo kuamua kuchukua jukumu la kuwasaidia watoto waliofaulu toka katika kitongoji cha Nyakiswa watano, Mwibagi sita, Nyamikoma tisa ambao jumla yake itakuwa ni watoto ishirini.

“Nimejaribu kushirikiana na watu kupitia ilani ya chama cha mapinduzi nilileta barua ili niweze kupata watoto nitakaoweza kuwasidia kupata elimu ya sekondari katika sekondari ya kyenyari kwani hata mimi nimepitia katika mazingira magumu” alisema….

“Katika kata hii kuna jumla ya watoto mia moja waliofaulu lakini kwa uwezo nilionao ninawaomba viongozi wa vijiji kusaidia kupatikana watoto ishirini kutoka kitongoji cha nyakiswa watano, mwibagi sita, nyamikoma tisa ambao jumla yao itakuwa ni watoto ishirini” aliongeza…

Muhochi ameongeza kuwa hivi sasa tayari ameshatuma barua kwa viongozi wa vijiji ili kuwapata watoto hao watakaoanza masomo katika sekondari ya kyenyari na hivyo kuwahimiza kuwa kabla ya feb 2 watoto hao wawe wameshapatikana.

“Mpaka feb. 2 mwaka huu naomba niwe nimeshapata majina ya watoto hao katika kata hii ambao watapatiwa     elimu shuleni hapo ili waweze kupata elimu itakayowasaidia katika maisha yao”

Awali  bw. Muhochi alimtupia lawama mtendaji wa kata ya kyenyari bw. Alfred Kitambala na kusema kuwa mtendaji huyo amekuwa ni mzigo kwa wananchi wa kata hiyo kwa kudidimiza shughuli za kimaendeleo kwa kutokamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa ya shule ya msingi mwibagi na maabara ya shule ya sekondari ya kyenyari.

Hata hivyo mjumbe huyo wa halmashauri kuu ccm kwa upande wa vijana (uvccm) wilayani butiama amemuomba mkurugenzi wa wilaya hiyo kumuondoa mtendaji Kitambala katika kata hiyo kutokana na kutowajibika katika majukumu yake ipasavyo.

“Kutokana na uzembe unaooneshwa na kiongozi huyu wa kata ninamuomba mkurugenzi wa wilaya amuondoe mtendaji huyu ambaye ameshindwa kabisa kutekeleza majukumu yake katika kata yetu” alimalizia………

Mwishooo…..





0 comments:

Post a Comment

 
Designed By | Wishes co |
Copyright © 2014. Jicho La Mdadisi - All Rights Reserved
Template Modify by
Proudly powered by Wishes INK