`

Home » » DJ CHOKA ATANGAZA KUACHANA NA KAZI YA U-DJ RASMI

DJ CHOKA ATANGAZA KUACHANA NA KAZI YA U-DJ RASMI



WAKATI VIJANA WENGI WAKITAMANI NA HATA KUJARIBU KUINGIA KATIKA TASNIA YA UDJ..DJ MAARUFU NCHINI DJ CHOKA AMETANGAZA KUACHANA NA KAZI HIYO RASMI HUKU AKIZITAHJA SABABU ZA KUACHANA NA KAZI HIYO ZAIDI JICHO LA MDADISI LINAKUPEKULIA HAYO.


Dj maarufu nchin dj choka ametangaza rasm kuachana na kazi hiyo aliyoitumikia kwa kipindi kinachokaribia miaka kumi huku akieleza kuwa sababu za kuachana na kazi hiyo kuwa ni ameona apumzike na kuendelea na kazi inayomuingizia kipato yani blog yake.

Kazi ya kudj wasanii ni kazi fulani nzuri lakini ni ngumu sana usipokuwa na hobby nayo, nimeifanya kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe yakupenda mziki na sikuwahi kulalamika mslahi ninayoyapata kwasababu niliifanya kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe hata napokuwa jukwaani nilikuwa nafurahia sana.

Lakini kwa kuwa kazi hii ya kuandika habari na kuonyesha kazi za wasanii wa hapa nchini ndio inayonilipa vizuri basi naona sina budi kupumzisha kimoja ili niendelee na kimoja.

Baada ya kupumzisha kazi yakudj kwenye majukwaa na kuwa dj sasa nitakuwa naendelea na kazi yakuvumbua vipaji vya wasanii ikiwa ni pamoja na kuendelea kutengeza mix tape zangu kama ilivyoada.

Ameongeza kuwa Msanii atakayemuhitaji kwa sasa basi ajue itakuwa kazi yakwenda kupiga picha show zake au kurecord show zake tu pindi atakapokuwa jukwaani. 

Mbali na hayo pia amesema ataendelea kupromoti mziki wa nyumbani na wasanii wake mpaka siku ya mwisho wa maisha yake.

Lakini mbali ya yote hayo hakuacha kuwazungumzia madj ambao ndityo kwanza wana malengo ya siku moja kuwa kama yeye amesema kuwa amefungua pia ukurasa mpya kwa kuwakaribisha dj's under ground waliopenda sana kazi hiyo na kukosa wapi kwa kuanzia.

Amesema atakuwa akiwapatia ushauri ikiwa ni pamoja na kuwafundisha njia za kuwa dj na hata njia za kuwachezesha wasanii wa hip hop na bongo flava pindi wawapo jukwaani jinsi ya kucheza nao na hata namna ya kulitawala jukwaani na kusababisha shngwe kwa mashabiki waliofurika.


Hata hivyo akamalizia kwa kusema kuwa anawapenda sana wadau wake wote wa DJCHOKA MUSIC kwani wao yeye aingekuwa hapo alipofikia.




                                                  CHOKA KATIKA POZI


0 comments:

Post a Comment

 
Designed By | Wishes co |
Copyright © 2014. Jicho La Mdadisi - All Rights Reserved
Template Modify by
Proudly powered by Wishes INK