`

Home » » MRADI WA TIBU HOMA KUNUSURU VIFO VYA WATOTO WALIO CHINI YA MAKA MITANO

MRADI WA TIBU HOMA KUNUSURU VIFO VYA WATOTO WALIO CHINI YA MAKA MITANO

Na Ahmad Nandonde,

Musoma.

Ili kuhakikisha maboresho ya huduma ya afya kwa watoto waliochini ya umri wa miaka mitano mradi wa tibu homa unaofadhiliwa na serikali ya watu wa marekani kwa kushirikiana na wizara ya afya na ustawi wa jamii imefanya mkutano wake kwa lengo la kujadili tathmini ya utekelezaji wa huduma hiyo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano mgeni rasmi katika mkutano huo ambaye pia katibu tawala wa mkoa bw. Benedict Ole Kuyan amesema kuwa mradi huo umelenga kupunguza vifo vya watoto vinavysababishwa na magonjwa yanayoambatana na homa kama vile numonia na kuhara na malaria kwa kuongeza ufanisi wa utambuzi na matibabu sahihi.

Amesema kuwa ili kuhakikisha vifo vinapungua ni wazi kuwa ipo haja ya kupatikana na ufikiwaji wa wa huduma za afya ya msingi, kuhakikisha huduma zinaboreshwa kwa watoto waliochini ya umri huo zinakuwa endelevu, ikiwa nim pamoja na kuishirikisha jamii kuboresha tabia ya kupata kinga na huduma za afya kila mara na hata mara baada ya mradi huo kumalizika.


Aidha Bw. Kuyan ameongeza kuwa vifo kwa watoto waliochini ya miaka mitano badi ni tatizo kubwa duniani hususani kwa nchi zilizopo kusini mwa jangwa la sahara kufuati takwimu ya sensa ya afya ya mwaka 2010 nchini inaonesha kuwa vifo vya watoto waliochini ya umri wa miaka mitano vimepungua toka 112 hadi kufikia 81 kati ya watoto 1000 waliozaliwa wakiwa hai.


Amesema kwa kanda ya ziwa idadi ya vifo imepanda kwa vifo 109 kati ya watoto 1000 waliozaliwa wakiwa hai na hii ni kutokana na kutokana na kushindwa kudhibiti mazalia ya mbu pamoja na maambukizi huku takwimu zikionesha kuwa mkoa wa mara ukikumbwa na kiasi kikubwa cha maambukizi ya malaria kinachofikia asilimia 25.

Akizungumza kwa niaba ya mganga mkuu wa mkoa bw. Wilson Winani mratibu wa malaria mkoani mara bi. Tukaye Lisso amewashukuru wawezeshaji mradi wa tibu homa na wizara ya afya na ustawi wa jamii kwa usaidia zoezi zima la kusaidia uboreshaji wa afya ya watoto waliochini ya umri miaka mitano.

Aidha bi. Lisso amesema kuwa ili kuenda sanjari na matakwa ya mradi huo hivi sasa wamedhamiria kutoa elimu kwa wahudumu katika suala zima la utoaji huduma za kiafya ikiwa ni pamoja na kuwataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao hospitalini pindi wanapogundua dalili za ugonjwa ndani ya masaa 24 ikiwa ni pamoja kuachana na tabia ya kujitibia wenyewe kabla ya kupatiwa vipimo toka vituo vya afya.

Kwa upande wake mganga mkuu wa halmashauri ya musoma dk. Genchwele Makenge amesema vifo vya watoto nchini bado ni changamoto kubwa ingawa serikali kupitia ngazi ya mkoa imeweka mikakati ya kuhakikisha vifo vya watoto chini ya miaka mitano inapungua kwa kunyunyuzia dawa ya ukoko kwa halmashauri tatu, matumizi ya chandarua, na utoaji wa matibabu sahihi vituoni.

Mkutano huo wa tathmini ya utekelezaji wa uboreshaji wa huduma za afya kwa watoto waliochini ya umri wa miaka mitano umefanyika jana katika ukumbi wa mikutano na mafunzo wa anglikana musoma.
 
Mwisho……….

0 comments:

Post a Comment

 
Designed By | Wishes co |
Copyright © 2014. Jicho La Mdadisi - All Rights Reserved
Template Modify by
Proudly powered by Wishes INK