Musoma.
Kufuatia
kuwapo kwa changamoto kubwa ya uhaba wa madawati katika shule nyingi zilizopo
katika manispaa ya musoma jumla ya madawati 357 yametolewa jana katika shule za
msingi zipatazo 20 katika manispaa hii.
Akizungumza
wakati wa kukabidhi madawati hayo meya wa manispaa ya musoma bw. Alex Kisurura
amesema kuwa mbali na kuwepo kwa shughuli nyingi za maendeleo lakini kamati ya
mfuko wa jimbo imeonelea kuanzia katika sekta ya elimu kwa kugawa madawati
katika shule.
Mbali
na madawati hayo 357 kutolewa kwa shule za msingi lakini pia jumla hya madawati
80 yametolewakwa shule za sekondari zipatazo kumi kwaajili ya kupunguza uhaba
wa madawati katika shule zilizopo ndani ya manispaa ya musoma.
Naye
mwalimu mkuu wa shule ya msingi Iringo 'A' Bi. Consolata Naftal ameushukuru
mfuko wa jimbo kwa msaada huo kwani wapo walimu ambao hawakupata msaada huo
mbali na msaada huo kuwa ni mdogo lakini utaweza tatizo hilo ingawa si kwa
kuondoa kabisa tatizo hilo kwani pamoja na msaada huo lakini bado shule yake
inahitaji madawati 101.
Zaidi
ya shilingi mil. 44 zimetumika katika utengezaji wa madawati hayo kwa shule za
msingi na zaidi ya shilingi mil. 24 kwa madawati ya shule za sekondari.


0 comments:
Post a Comment