`

Home » » CCM YAAHIDI KUENDELEA KUWAFIKISHA VIONGOZI WAZEMBE KWENYE VIKAO VYA KIMAADILI.

CCM YAAHIDI KUENDELEA KUWAFIKISHA VIONGOZI WAZEMBE KWENYE VIKAO VYA KIMAADILI.

Rorya:

Chama cha mapinduzi (ccm) kimesema hakitasita kuwasema na kuwafikisha kwenye vikao vya maadili watumishi ambao watashindwa kufanya kazi zao na kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama hicho na kupelekea kulalamikiwa na wananchi.

Akizungumza katika mkutano wa maazimisho ya miaka 37 ya chama cha mapinduzi ccm wilayani rorya,mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa geita Joseph Kasheku  amesema wataizingatia kauli ya rais jakaya kiwete aliyoitoa mkoani mbeya kutomuonea aibu mtumishi na kufatilia kwa karibu utekelezaji wa ilani.

Kasheku amesema kamwe hawatokubali kuona watumishi wazembe na wanaojiingiza kwenye siasa kukwamisha shughuli za maendeleo kwa kutosimamia miradi huku shutuma zikielekezwa kwa serikali ya ccm.

Msukuma amesema katika siku za hivi karibuni kumeibuka taarifa za kuhusu chama cha mapinduzi (ccm) wilayani rorya kulalamikia utendaji kazi wa mkuu wa wilaya hiyo pamoja na mkurugenzi na kusema ili kazi ziweze kwenda ni lazima viongozi wa ccm wawe wakali katika kusimamia ilani.

Mwenyekiti huyo wa ccm mkoani geita ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maazimisho hayo yaliyofanyika kiwilaya katika uwanja wa nyanduga, amewataka viongozi wa ccm wilaya ya rorya kutokusita kuzungumza kila wanapoona uzembe wa watumishi.

Mwisho..... 


0 comments:

Post a Comment

 
Designed By | Wishes co |
Copyright © 2014. Jicho La Mdadisi - All Rights Reserved
Template Modify by
Proudly powered by Wishes INK