`

Home » » MTOTO ALIYETEKWA MUSOMA APATIKANA NJAMA ZA WATEKAJI ZAGONGA MWAMBA

MTOTO ALIYETEKWA MUSOMA APATIKANA NJAMA ZA WATEKAJI ZAGONGA MWAMBA



Na Ahmad Nandonde,
Musoma.

JESHI la Polisi mkoani mara limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili waliojulikana kwa majina ya Vicent Range Magesa umri 19 na Erick Abbas Anthony (21) kwa kosa la kumteka nyara mtoto Diana Meshaki mwenye umri wa miezi 7 mtoto wa bi. Gaudioza Meshaki (27) kabila mhaya mkazi wa mtaa wa nyamiongo kata ya makoko wilayani muisoma mkoani mara.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 09/ 01/ 2015 kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa bw. Phillip Kalangi alisema kuwa mnamo tarehe 3 january mwaka huu majira ya saa tatu asubuhi katika mtaa wa nyamiongo kata ya makoko mjini musoma nyumbani kwa bi. Gaudioza Meshaki, binti wa kazi aliyejulikana kwa jina la Paulina Sobe (17)  kabila mkurya mwenyeji wa getabwega nchini Kenya alimtorosha mtoto Diana na kutyokomea naye nchini Kenya.

Kamanda Kalangi alisema kuwa yalipofika majira ya saa kumi na mbili kamili jioni mama mzazi wa mtoto huyo alipokuwa kaityokea kazini kwake alikuta mfanyakazi wake na mtoto wake hawapo nyumbani aliamua kutoa taarifa kwa majirani ambao waliwatafuta bila mafanikio na ndipo uamuzi wa kutoa taarifa katika kituo kikubwa cha polisi cha musoma.

Aidha Kalangi alisema ilipofika tarehe 4 January mama wa mtoto huyo alipigiwa simu na watu wasiojulikana wakimtaka awape kiasi cha shilingi miloni tatu na kama asipotoa kiasi hicho cha fedha basi wangemuuza mtoto huyo kwa watu wanaotafuta watoto.

Hata hivyo kamanda huyo alisema kuwa jeshi la polisi bado linaendelea kumsaka Paulina Sobe kwa tuhuma za kumtorosha mtoto huyo pamoja watu wengine waliohusika na uhalifu huo ili wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya dola huku akiwataka wazazi kuwa makini pindi wanapoajiri wafanyakazi za ndani kwa kuwa na kumbukumbu za wanapotoka, pamoja na kuwatambulisha kwa viongozi wa maeneo husika wakiwamo wamiliki wa nyumba wanazoishi ili iwe rahisi kuwafahamu ndugu zao na mahala wanapoishi ili iwerahisi kuwapata pindi kunapotokea matataizo kama hayo.

Mama mzazi wa mtoto huyio bi. Gaudioza amesema alilishukuru jeshi la polisi mkoani mara na jeshi polisi kanda maalumu Tarime/Rorya kwa kushirikiana na jeshio la polisi nchini kenya kwa kufanikisha kumpata mtoto wake.

Aidha alielezea namna watekaji hao walivyuompigia simu huku wakimtaka awapatie fedha shilingi milioni tatu na mama huyo alipowauliza wanazitaka hizop pesa kwaajili gani wakamjibu ili wamerejeshe mtoto wao na asipotoa basi watamuuza kwa watu wengine ambao wanahitaji watoto kwani wapom wengi wanaohitaji watoto.

Kwa hatua hiyo na ujasiri mkubwa mama huyo alityoa taarifa kwa jeshi la polisi mkioani mara kwa kushirikiana na kanda maalumu tarime/rorya na kasha kuzifuatilia namba hizo ambazo tariifa za za mwisho kabla simu hiyo haijazima mawasiliano yaliishia sirari kwamaana kuwa watu hao walikuwa wakitorokea nchini Kenya.

“Baada ya kufuatilia mawasiliano tuligundua watuhumiwa hao walielekea nchini Kenya na hivyo nikaamua kumpigia simu ndgu yangu aliyeko sirari ili awasiliane na jeshi la polisi la Kenya kwa kushirikiana na jeshi la polisi kanda maalumu tarime /rorya amabao nao walifanikisha kuwakamata wakiwa na mtoto wangu na hivyo wakawachukuliwa na jeshi la polisi mkoani hapa,”alimizia Bi. Gaudioza.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi waliofurika  katika kituo kikubwa cha polisi mjini musoma Bi. Ghati Msamba alilishukuru jeshi la polisi kwa kufanikisha kupatikana kwa mtoto huyo na kuongeza kuwa tabia za wasichana wakazi kufanya ukatili unaofanana na huo unawanyima amani wazazi hali inayopelekea wakati mwengine wazazi kushindwa kufanya kazi zao za kujiingizi akipato nyuimbani.

Pia alizungumzia tabia ya baadhi ya majirani kuwa ndiyo sababu ya kuwapa viburi wafanyakazi wa ndani huiku wakiwapa maneno ya uongo ili watoto hao warubunike na kukimbia na hata kufanya vitendo viovu.

Mwishoo….


                                   KAMANDA PHILIP KALANGI AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI
                       KAMANDA PHILP KALANGI AKIWA AMEMBEBA MTOTO DIANA
KAMANDA WA JESHI LA POLISI MKOANI MARA PHILP KALNGI AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI
 MTOTO NA MAMA YAKE PICHANI W
MAMA WA MTOTO ALIYETEKWA NA MWANANE AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI.
        MASHUHUDA WALIOFURIKA KITUO KIKUBWA CHA POLISI MJINI MUSOMA

0 comments:

Post a Comment

 
Designed By | Wishes co |
Copyright © 2014. Jicho La Mdadisi - All Rights Reserved
Template Modify by
Proudly powered by Wishes INK