`

Home » » MEZ B AUCHUKIA MUZIKI TANGU NGWEAH ALIPOFARIKI.

MEZ B AUCHUKIA MUZIKI TANGU NGWEAH ALIPOFARIKI.

Mez B
Mez B   ni kati ya wasanii ambao walifanya kazi kwa ukaribu sana na marehemu  alberty mangwea , (ngweah)  na kufanikiwa kutoa  baadhi ya ngoma wakiwa pamoja ,  amesema amejikuta  akiuchukia sana  muziki wa kitanzania baada ya ngwea kufariki  tu , na hii ni badaa ya kuona kama amepoteza kila kitu katika muziki kiasi cha wakati mwingine kujikuta na mfadhaiko ( stress) kila anapomkumbuka  Ngweah.
                                          
Marehemu Albert Mangweah

Mez B aliyasema hayo wakati akizungumza na blog  ya  delduero .blogspot .com   kwa njia ya simu kuhusiana na mipango yake ya kimuziki  na namna ambavyo  amejipanga tena kwa mwaka huu baada ya  mwaka jana kuachia ngoma iliyokwenda kwa jina la kidela .

“patty najua unajua jinsi ambavyo mimi na marehemu cowboy  tulivokuwa , kwa hiyo kiukweli wakati mwingine nakuwa na stress sana kila ninapomfikiria marehemu alberty mangwea , maana nahisi  kifo chake kilinichanganya na kunivuruga  kimuziki kiasi cha mimi kuona  kama nimepoteza  kila kitu  yaani  katika hili gemu.”alisema  MEZ B

katika hilo pia  akiuzungumzia muziki wa Tanzania kwa sasa  na jinsi ulivyo , mez b alisema muziki  wa Tanzania kwa sasa ni mzuri   lakini  haupo fair kabisa  kiasi cha kuendelea kuwaumiza wanaojua na kuwaacha katika mateso   na hali ngumu ya kimaisha , kutokana  uarasimu wa wachache wenye nguvu ya  fedha  kuendelea kuhit  hata kama ni wabovu na wale wasio na fedha hata kama ni wazuri  wakiachwa .

“Muziki  hauko fair kabisa , ambao tunauwezo mkubwa sana  bado  tunakuwa katika  hali ngumu ya kimaisha  na hali ya umasikini wa hali ya juu , lakini wale wasiokuwa na uwezo wa kufanya vizuri katika gemu,lakini wana uwezo wa kifedha ndo hao wamekumbatia gemu  na hakuna wachofanya zaidi ya kupewa promo   kiasi cha kuwaacha wasio na uwezo wa kifedha kuzidi kuteseka  au kutokusikika ,  na patty  nakwmabia kama hii hali itaendelea inavyoendelea we jua tu muziki wetu kila siku tutakuwa tunayasikia yale yale  kutoka kwa wale wale”alisema   Mez B
                                   

 Marehemu Ngwea alifariki dunia may 28 2013 Johannesburg South Afrika alikokuwa kwaajili  ya kufanya show, ambapo kilikua ni kifo cha ghafla kwa sababu usiku kabla ya kulala aliagana vizuri na Watanzania wenzake kijiweni tena akaahidi kurudi Afrika Kusini baada ya kipindi cha Ramadhani.

Kabla ya kifo chake tayari Ngwea alitakiwa kurudi Tanzania lakini akaahirisha safari yake mara tatu mfululizo ili aendelee kuwepo Afrika Kusini ambako alimwambia Bushoke kwamba amepata mtu wa kumlipia ada hivyo angerudi Afrika Kusini hivi karibuni ili aanze masomo ya muziki.
                               



0 comments:

Post a Comment

 
Designed By | Wishes co |
Copyright © 2014. Jicho La Mdadisi - All Rights Reserved
Template Modify by
Proudly powered by Wishes INK