`

Home » » YAELEZWA KUWA SABABU YA KUFELI KWA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA KATIKA HALMASHAURI YA MUSOMA KUNATOKANA NA VIBOKO MASHULENI.

YAELEZWA KUWA SABABU YA KUFELI KWA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA KATIKA HALMASHAURI YA MUSOMA KUNATOKANA NA VIBOKO MASHULENI.

Musoma.

IMEELEZWA kuwa sababau kubwa inayochangia wanafunzi kufeli masomo ya kuingia kidato cha kwanza ni kunatokana na mgogoro uliopo baina ya wazazi na walimu hususan wanapotoa adhabu kwa wanafunzi hao.

Kauli hiyo imetolewa leo na madiwani wa halmashauri ya Musoma kwenye kikao cha baraza kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Diwaniwa wa Viti Maalum bi. Debora Mogaya alisema kuwa kinchochangia ni wazazi kutotoa ushiriano na walimu kwa kuhakikisha watoto wanafika shuleni na sio walimu kukaa muda mrefu kama alivyosema diwani wenzake wa kata ya Bulinga Mambo Japan  kuwa walimu kukaa muda mrefu na walimu kupewa vyeo vya ualimu Mkuu wa Shule za Msingi  bila kuwa na sifa hiyo.

“Wanafunzi waliofelini wale ambao hufanya utoro wa kutoenda shuleni mara kwa mara ,hivyo inatupasa sisi viongozi tufanye mazungumzo na wazazi na walimu wetu ili tubaini tatizo la elimu’’,AlisemaDiwani Debora.

“Wazazi na  walimu wetu  ni mgogoro sana ambayo inamfanya mwalimu kuwa na ugumu wa utendaji wa kazi hasa pale anapomuadhibu mwanafunzi”,alisisitiza tena.

Naye diwani wa kata Bukumi Chomya Ndege alimuomba Afisa elimu wa Halmashauri hiyo kuwasimamia walimu ili kutatua  migogoro na kuboresha sekta ya elimu ambayo ni msingi  wa maisha wilayani humo.

“Mitaala nayo inachangia ,zaman iilikuwa aihamihami hivyo tunaiomba serikali kuu kulingalia hili kwani inachangia  pia’’,Aliongeza Ndege.

Awali hoja hiyo ilitaka kuleta mtafaruku baina ya Diwani wa kata Bulinga Mambo na Afisa Elimu wa halmashauiri Magesa , diwani akidai   kuwa walimu Wakuu wakipewa  vyeo hivyo bila kuwa na sifa kutokana na Afisa elimu huyo kupewa rushwa ambapo Afisa Magesa alimtaka diwani huyo kumuomba radhi ama kumdhibitishia ukweliwa jambo hilo.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo amewaomba madiwani hao kufuata taratibu ni kanuni za uendeshaji wa vikao ili kutatua mapungufu yanayojitokeza na  kwamba kikao cha baraza la madiwani ni kujenga na sio kubomoa hivyo amewataka kutumia busara zao kwa lugha ya ustaraab badala ya kutumia lugha za matusi  kwa watumishi.

Amemtaka Diwani Mambo kumuomba radhi Afisa elimu huyo ilikuendelea ama kuweka kikao vizuri  ambapo diwani huyo alimuomba  radhi na kikao kikaendelea kuda ikuwa Afisa Magesa ndiye wa kulaumiwa kwani yeye ndiye mtendaji Mkuu katika Sekta hiyo ya elimu.
  
Kwa  upande  wa  Mkurugenzi  Mtendaji  Fidelica Myovela  alisema  wamejiwekea  mkakati wa kuzungumza na walimu na kwamba kutokana mila na desturi zinasababisha kuwa kwamisha  zinawavyunja moyo hali inayowasabisha  kuomba  uhamisho.

Mwisho.................


0 comments:

Post a Comment

 
Designed By | Wishes co |
Copyright © 2014. Jicho La Mdadisi - All Rights Reserved
Template Modify by
Proudly powered by Wishes INK